Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Abjadi, abtathi au alfabeti

Posted on By Harun Mbijiwe 6 Comments on Abjadi, abtathi au alfabeti

Abjadi ni nini?

Abjadi au alfabeti ni sauti 30 za lugha ya Kiswahili. Hata hivyo tukirejelea kamusi kuu ya TUKI tutapata 31. Herufi C, Q na X hazipo katika alfabeti. Tazama herufi sifuatazo:-

  • a, b, ch, d, dh, e, f, g, gh, h, i, j, k, kh, l, m, n, ng’, ny, o, p, r, s, sh, t, th, u, v, w, y, z.
  • Herufi Kh imeongezewa katika kamusi ya tuki.

Tunaweza kugawanya herufi hizi mara mbili.

Voweli au irabu (5)

a, e, i, o, u

Konsonanti (25)

b, ch, d, dh, f, g, gh, h, j, k, kh, l, m, n, ng’, ny, p, r, s, sh, t, th, v, w, y, z.

Silabi

Silabi huundwa kwa kutumia herufi ya konsonanti na voweli moja. Hutamkwa kama sauti moja. Kwa mfano:

  • ch + a = cha
  • m + e = me
  • z + i = zi
  • dh + o = dho

kwa hivyo:

Neno hobelahobela lina silabi 6 – ho + be + la + ho + be + la

Neno mwanafunzi lina silabi 4 – mwa + na + fu + nzi  

Sauti

Sauti za Kiswahili ni abjadi au alfabeti ya Kiswahili. Neno lolote la Kiswahili  huundwa kwa sauti hizi. Zinaweza kuwa konsonanti au voweli.

Mifano katika maneno:

Neno kiatu lina sauti (5), dhahabu lina sauti (5) ilhali neno segemnege lina sauti (5)

Hivyo ni kusema tunahesabu kila herufi ya abjadi kivyake inapopatikana au kujitokeza mara ya kwanza:

  • k–i–a–t–u (5)
  • dh–a-h-a-b-u (5)
  • s-e-g-e-m–n-e-g-e (5)

Sauti Ghuna

Sauti hizi zikitamkwa hughuna kwa ndani. Sana sana ukiziba masikio utaisikia unapotamka sauti yenyewe mgurumo wa ndani unajitokeza.

Sauti hizi ni kama vile: b, d, dh, g, j, m, n, ng’, ny, v, w, y, z (13)

Sauti Sighuna

Sauti hizi zikitamkwa hasighuni yaani koo haitikisiki. Sana sana ukiziba masikio utaisikia unapotamka sauti yenyewe haitakuwa na mgurumo wa ndani.

Sauti hizi ni kama vile: ch, f, h, gh, l, k, p, r, s, sh, t, th. (12)

Sentensi ya ukumbusho: Sh! Chifu Seth tukupora ghala hii si-ghuna

Mwanagenzi akitaja sentensi hii atajikumbusha sauti sighuna.

Silabi Changamano

Silabi au sauti hii huundwa kwa herufi zaidi ya moja hasa konsonanti. Hutamkwa kwa pamoja na husikika zikiwa sauti moja.

Mfano katika maneno: Changamano, Muumba, kichala, dhana, ghala.

Silabi Mwambatano

Kuambatana ni kufuatana kwa mambo moja baada ya jingine. Sauti hii huundwa kwa herufi mbili au zaidi na hutamkwa moja baada ya nyingine.

Mfano katika maneno: mwambatano, mwana, kinywaji, nywele, mbwembwe. Msengwe, mfuko.

 

Maswali ya Alfabeti

  1. Herufi ch, dh, gh, ng’, ny, huitwa ___________________
  2. Herufi a, e, i, o, u huitwa _________________________
  3. Vitamkwa ambavyo huundwa na herufi sifuatazo kama ifuatavyo – ng’ + a = ng’a , z + a = za – Kwa jina moja ni ___________________
  4. Unapotaja herufi kama ifuatavyo – m-a-h-a-l-i – ili kuweza kuhesabu , tunasema unahesabu ___________________
  5. Sauti g, ny, v, z, ni sauti _________________
  6. Sauti f, h, l, k ni sauti ___________________
  7. Neno dhamana lina silabi zinazoitwa ___________________
  8. Neno mwao lina silabi zinazoitwa ______________________
  9. Neno jingine la abjadi ni ________________ au ______________

<<<<<< Majibu ya Maswali ya Abjadi >>>>>>>

Zoezi la ziada

[ays_quiz id=”2″]

Post Views: 149
Sarufi

Post navigation

Previous Post: Aina za Vihisishi (Interjections)
Next Post: Vitendawili

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme