Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Aina ya Vielezi (adverbs)

Posted on By 6 Comments on Aina ya Vielezi (adverbs)

Kielezi ni neno linaloelezea zaidi kuhusu kitenzi, kivumishi au kielezi.

a) Vielezi wakati (Adverbs of time)

Tutaonana mwakani.
Mzee mlevi alifika usiku wa manane.

b) Vielezi mahali (Adverbs of place)

Wameondoka kwenda cheteni.
Ndege wameingia kiotani.

c) Vielezi jinsi au namna (Adverbs of manner)

Amecheza kwa ustadi.
Walimaliza chakula haraka.

d) Vielezi kiigizi (Adverbs of interjection)

Alianguka mchangani tifu!
Njia imenyoka twa!

e) Vielezi mkazo

Tumeelezwa mambo yote dhahiri shahiri.
Mama alimchapa mwanawe bure bilashi.

f) Vielezi namna vikariri/takriri

Alibebwa hobelahobela.
Anatembea asteaste.

g) Vielezi idadi au kiasi (Adverb of degree)

Aghalabu tutakuwa tukionana.
Amekula matunda mengi.

h) Vielezi tashibihi

Alijuta kama Filauni.
Walivumilia mateso kama watumwa.

i) Vielezi kiulizi (interrogative adverb)

Mtaniletea nini?
Ameondoka kwenda wapi?

Maswali ya Vielezi

Post Views: 151
Sarufi

Post navigation

Previous Post: Jinsi ya kujibu kifungukate
Next Post: Aina za Vihisishi (Interjections)

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme