Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Aina za Vihisishi (Interjections)

Posted on By 6 Comments on Aina za Vihisishi (Interjections)

Vihisishi ni maneno ya kuonyesha hisia mbalimbali za mzungumzaji. Alama ya hisi hutumika baada ya kiingizi! Tazama baadhi ya viigizi vifuatavyo vilivyopangwa kulingana na hali tofautitofauti:

Dharau

Mifano: Chub!Chup! Ebo! Khaa! Kefle! Po! Pukachaka! Nyoo! Us! Wee! Zii!

Furaha / Shangwe

Haleluyah! Ewaa! Chabaa! Oyee!
Oyaa! Huree! Shabash!

Heshima

Tafadhali!

Huruma

Jamani! Pole! Maskini!

Huzuni

Pole! Ole!

Kuchoka

Oofu!

Kuelewa

Alaa! Ahaa!

Kukanusha

Aka! Ata! Hasha! Hata! La!

Kukataa

Abadan kataan! La! Hasha!
Kamwe! Hapana! Ng‘o!

Kuitikia

Abee! Beka!

Kukemea

Ebo! Wee!

Kukubali

Barabara! Enhe! Haya! Hewaa! Hewala! Naam! Ohoo! Taib! Sawa! Taibu!

Kulaani/kukashifu

Do! Pukachaka! Zii!

Kulaani shetani

Audhubillahi!

Kuomba msaada kwa Mungu

Yarabi maskini!(msaada wa Mungu), Yarabu Stara! (ulinzi wa Mungu)

Kuomba samaha hasa unapotaka kusema jambo ambao linaweza kuudhi

Ashakum!

Kusifu Mungu

Halleluyah!

Kutia moyo

Harambee! Halumbe! Twende!

Majuto

Kama! Falaula! Lau! Laiti! Ole wangu!

Mshtuko

Aisee! Afanaleki! Alaa! Jamani!

Lo! Toba!

Mshangao

Ah! Aka! Ala! Ajabu! Cho! Do! Ewe! Haya! Kumbe! Lo! Lakwata! Masalale! Oho! Salala!

Shukrani

Asante! Alhamdulilahi!

Shaka

Eti!

Uchungu

Aa!,

Woga

Mama wee! Mungu wangu!

Maswali ya Vihisishi

Katika vikundi vya maneno uliyopewa 1-10 sema ni hali gani ya viigizi imetumika.

  1. Abadaan! Kamwe!
  2. Mama wee! Mungu wangu!
  3. Aka! Lakwata!
  4. Pole! Ole!
  5. Hasha! Ng’o!
  6. Jamani! Maskini!
  7. Chup! Zii!
  8. Do! Pukachaka!
  9. Barabara! Taib!
  10. Yarabi stara! Yarabi maskini!
Post Views: 163
Sarufi

Post navigation

Previous Post: Aina ya Vielezi (adverbs)
Next Post: Abjadi, abtathi au alfabeti

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme