Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Jinsi ya kujibu kifungukate

Posted on By Harun Mbijiwe 6 Comments on Jinsi ya kujibu kifungukate

Mwanafunzi aelewe kuwa kifungukate au kiasho hutahini mambo kadhaa ya sarufi, kusikiliza na kuzungumza, msamiati na ufahamu wa maendelezo tofautitofauti ya maneno ambayo wakati mwingine huendelezwa visivyo. Mambo haya yote huwa yanajitokeza lakini linalochukua sehemu kubwa ni sarufi.

Mwanafunzi anaposoma kifungukate anapaswa aangalie:

Nyakati

Kifungu kimeandikwa kwa wakati gani kwa mfano:- li wakati uliopita, na wakati uliopo, ta wakati ujao nk.

Ngeli

Atazame aaone ni ngeli gani zimetumika katika kila sentensi ili aweze kuteua viambishingeli vinavyofaa. Km. Mama alikuwa ____1_____ sokoni magari ____2___ kwetu nyumbani. Majibu yanapaswa kulenga nomino mama na magari ambazo ni nominokuu katika sentensi.

Virejeshi

Mwanafunzi ajue kuwa virejeshi hutahiniwa kwa sababu huleta msisitizo katika sentensi husika au kurejelea nomino fulani katika sentensi yenyewe.

Tazama: Kitabu kilichokuwa kikizungumziwa ni hiki. Rejeshi o kati imetumika kuleta msisitizo na kuifanya sentensi iwe sawa kisarufi.

Nafsi

Mwanafunzi aajue wahusika wanaozungumziwa ni kina nani. Ajue atarejelea mtu wa kwanza, wa pili au wa tatu. Km. ‘_____ kwenu kesho nikuone.’ Karani alisema. Nikitumia vijalizo(atakuja, nitakuja, wangekuja) jibu sahihi ni nitakuja kwa sababu mzungumzaji yu katika nafsi ya kwanza umoja na kiambishi ni kinapaswa kutumika.

Msamiati

Mwanafunzi ajue na atambue msamiati uliotumika katika kifungu. Kwa mfano shuleni hatuna watu na nyumba bali wanafunzi, ofisi, walimu, walinda lango, bwalo, madarasa, ofisi, walimu, madaftari nk.

Shambani atapata mboji, makoongo, matuta, tikitimaji, pilipili mboga, pilipili hoho, tololi, nk

Maendelezo

Maendelezo ya majina yanayoendelea visivyo hutahini wa sana katika kifungukate. Mifano: maakuli na mankuli, maandazi na mandazi, kiamshakinyua na kiamsha kinyua, makazi na makaazi, kwa sababu na kwasababu, dhahabu na thahabu, ghorofa na gorofa nk.

Viunganishi

Maneno ya kuunganishia sentensi hutahiniwa sana katika kifungukate. Mwanafunzi aelewe maana na visawe vya viunganishi ili iwe rahisi kwake kujibu maswali atakayokutana nayo. Mfano: sembuze au seuze, fakaifa, kefu huonyesha kulinganisha mambo mawili la kwanza likiwa ngumu kuliko la pili.

Katika sentensi:- Umemla mbuzi mzima seuze sungura.

Kusikiliza na kuongea

Sehemu hhii hutahini sehemu mbalimbali za kusikiliza na kuongea. Mwanafunzi ajikakamue kuelewa kwa kiwango kikubwa:-

  1. Tashibihi
  2. Methali
  3. Nahau
  4. Semi
  5. Visawe
  6. Vitawe
  7. Vitate nk

Post Views: 148
Mawaidha ya Ufundishaji

Post navigation

Previous Post: Majibu ya maswali mbalimbali
Next Post: Aina ya Vielezi (adverbs)

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme