Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Methali Zinazolandana

Posted on By Harun Mbijiwe 6 Comments on Methali Zinazolandana

Methali ni usemi wa kisanii wa kimapokeo unaofikiriwa na jamii kuwa kweli na unaotumiwa kufumbia au kupigia mfano na huwa umebeba maana pana kuliko maneno yenyewe yanayotumiwa. ( Maelezo kutoka katika Kamusi ya TUKI uk 240)

Kwenda na wakati

  1. Aendaye kisimani wa kwanza hunywa maji maenge.
  2. Chuma kiwahi kingari moto.
  3. Ivute ngozi ingali mbichi.
  4. Kambare mkunje angali mbichi.
  5. Samaki mpatilize angali mbichi.
  6. Tikiti ni moto wa kwanza.
  7. Udongo upatilize ungali maji.
  8. Udongo uwahi uli maji.

 Thadhari dhidi ya tamaa

  1. Bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi.
  2. Chako ni chako cha mwenzio si chako.
  3. Fuata nyuki ukafie mzingani.
  4. Mkate mkavu wa nyumbani ni bora kuliko nyama ya pengine.
  5. Mla kwa miwili hana mwisho mwema.
  6. Mpanda farasi wawili hupasuka msamba.
  7. Mtaka yote hukosa.
  8. Mwangata mbili moja humponyoka.
  9. Njia mbili zaumiza.
  10. Njia mbili zilimshinda fisi.
  11. Tamaa ilimwua fisi.
  12. Tamaa mbele mauti nyuma.
  13. Usiache kunanua kwa kutega.
  14. Usisafilie nyota ya mwenzio.

Umoja na ushirikiano

  1.  Jifya moja haliinjiki chungu.
  2. Ukuni mmoja hauwaki mekoni.
  3. Kichango ni kuchangizana.
  4. Kidole kimoja hakivunji chawa.
  5. Kijiti kimoja hakisimamishi jingo.
  6. Kinga na kinga ndipo moto uwakapo.
  7. Kofi hazilii ila kwa viganja viwili.
  8. Mafiga mawili hayaivishi chungu.
  9. Mkataa wengi ni mchawi.
  10. Mkono mmoja hauchinji ng’ombe.
  11. Mkono mmoja hapambi ngoma.
  12. Mkono mmoja haushindi vita.
  13. Mkono mmoja haubebi.
  14. Mtu ni watu.
  15. Nguzo moja haijengi nyumba.
  16. Nyege ni kunyegezana.
  17. Tembe na tembe huwa mkate.
  18. Ukiujua huu hujui ule.
  19. Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu.
  20. Vitanga vya mkono hunawishana.
  21. Watu ni kikoa.
  22. Wawili si mmoja.

 Nasaha ya kutia bidii

  1. Mchumia juani hulia kivulini.
  2. Achanikaye kwenye mpini hafi njaa.
  3. Zohali ni nyumba.
  4. Ajizi ni nyumba ya njaa.
  5. Auguaye huaguliwa.
  6. Bahati ni chudi.
  7. Kawia ufike.
  8. Kilicho baharini kakingoje pwani.
  9. Mgagaa na upwa hali wali mkavu.
  10. Mtaka cha mvunguni sharti uiname.
  11. Mvumilivu hula mbivu.
  12. Mwana mtukutu hali wali mtukutu.
  13. Mwenye shoka hakosi kuni.
  14. Ukitaka la waridi sharti udhurike

 Tahadhali dhidi ya kuhadaika kwa sura ya nje

  1. Vyote viowevu si maji.
  2. Hakuna masika yasiyokuwa na mbu.
  3. Kizuri hakikosi ila.
  4. Mchele haukosi ndume.
  5. Penye urembo ndipo urimbo.
  6. Sihadaike na rangi tamu ya chai ni sukari.
  7. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.
  8. Uzuri wa kuyu ndani mabuu.
  9. Vyote ving’aavyo si dhahabu.
  10. Nasaha ya kutokata tamaa
  11. Baada ya dhiki faraja.
  12. Kenda karibu na kumi.
  13. Mla cha uchungu na tamu hakosi.
  14. Mvumilivu hula mbivu.
  15. Penye nia na milango ipapo.
  16. Penye nia pana njia.
  17. Taabu ya leo ni furaha ya kesho.
  18. Tembe kwa tembe huwa mkate.
  19. Tone kwa tone huwa mchirizi.
  20. Umemla ng’ombe mzima husishindwe na mkia.
  21. Zito hufuatwa na jepesi.
  22. Wimbi kali hufuatwa na shwari.

 Tahadhari dhidi ya kucheka kasoro za wengine

  1. Ajabu ya kibogoyo kumcheka mapengo.
  2. Ajabu ya kondoo kucheka kioo.
  3. Ajabu ya ngamia kucheka nundu ya ng’ombe.
  4. Ajabu ya kipofu kumcheka chongo.
  5. Nyani haoni kundule.
  6. Nyani huchekana ngoko.

 Nasaha ya kufuata udugu

  1. Damu ni damu si kitarasa.
  2. Cha ndugu huliwa na ndugu.
  3. Damu ni nzito kuliko maji.
  4. Isipowasha hunzaye.
  5. Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa naye.
  6. Ndugu chungu jirani mkungu.
  7. Ndugu mbaya humshinda rafiki mzuri.
  8. Ndugu mtambie usimkalie.
  9. Ndugu mui heri kuwa naye.
  10. Ndugu ni kufaana si kufanana.
  11. Udugu wa nasi hukutania pakachani.
  12. Wa kuume haukati wa kushoto.

Nasaha ya kutenda wema

  1. Jaza ya hisani ni hisani.
  2. Kumpa mwenzio si kutupa.
  3. Kwendako hisani hurudi hisani hakurudi nuksani.
  4. Mtenda jamala hulipwa jamala.
  5. Wema hauozi.
  6. Tenda wema huende zako.

Tahadhari dhidi ya maringo

  1. Usione Kwenda mbele kurudi nyuma si kazi.
  2. Pavumapo palilie si kazi kudamirika.
  3. Aliye juu mngojee chini.
  4. Mpanda ngazi hushuka.

 Tahadhari dhidi ya kudharau ulivyo navyo

  1. Usione tanga la nguo ukasahau la miyaa.
  2. Baya baya lako si jema la mwenzio.
  3. Bura yangu siibadili na rehani.
  4. Usiache mbachao kwa msala upitao.
  5. Usidharau dafu embe ni tunda la msimu.
  6. Usile na sahani ukasau bunguu.
  7. Usisahau ubaharia kwa sababu ya unaodha.

Nasaha ya kuwa na subira

  1. Haraka haraka haina Baraka.
  2. Kakaka haina Baraka.
  3. Kawia ufike.
  4. Mbio za kasa si mbio lakini humfikisha aendapo.
  5. Mbio za sakafuni huishia ukingoni.
  6. Mstahimilivu hula mbivu.
  7. Mnywa maji kwa pupa kiu yake i pale pale.
  8. Mvumbika mbichi hula mbivu.
  9. Mwenda pole hajikwai.
  10. Mwenye pupa hadiriki kula tamu.
  11. Asubiriaye hajuti.
  12. Polepole ya kobe humfikisha mbali.
  13. Poepole ndio mwendo.
  14. Samba mwenda kimya ndiye mla nyama.
  15. Subira huvyaa mwana mwema.
  16. Urumi  haikujengwa kwa siku moja.

Tahadhari dhidi ya kudharau waliokufaidi

  1. Mchana ago hanyeri huenda akauya hapo.
  2. Usimcheke mamba kabla ya kuvuka mto.
  3. Usitukane wakunga na uzazi ungalipo.
  4. Visima vya zamani havifunikwi.
  5. Daraja lililokuvusha usilitukane.

Anayejua jambo vizuri ni aliye karibe nalo

  1. Siri ya mtungi aijuaye kata.
  2. Aibu ya maiti aijuaye ni mwosha.
  3. Adhabu ya kaburi aijuaye ni maiti.

Kutosikia mawasia na majuto

  1. Asiyeangalia huishia ningalijua.
  2. Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.
  3. Asiyesikia huishia ningalijua.
  4. Asiyesikia husafiria mtumbwi wa mfinyanzi.
  5. Asiyesikia la mkuu huvunjika guu.
  6. Asiyesikia la wakuu hufikwa na makuu.
  7. Kiburi majuto.
  8. Kilio si dawa.
  9. Maji yakimwagika hayasoleki.
  10. Majuto ni mjukuu mwisho huja kinyume.
  11. Mdharau mwiba huota tende.
  12. Msiba wa kujitakia hauna kilio.
  13. Mwiba wa kujidunga hauambiwi pole.
  14. Palipo wazee hapahabiki jambo.
  15. Radhi ya wazee ni fimbo kubwa kwa mwanadamu.
  16. Sikio halipwani kichwa.
  17. Mkataa pema pabaya pamwita.

Tahadhari dhidi ya kujiusisha na mambo yasiyokuhusu

  1. Aliye kando haangukiwi na mti.
  2. Samli ya pemba haimpati mtu macho.
  3. Pilipili iliyo shambani yakuashiani.

Akiba

  1. Akiba haiozi.
  2. Akiba ni iliyo kibidoni.
  3. Akiba si mbi ingawa ya kumbi siku ya kivumbi katia motoni.
  4. Hakuna hakiba mbovu.

Tahadhari kwa kuzuia wengine wasinufaike

  1. Jivu usilolilalia usilipigie jibwa.
  2. Mavi usiyoyala wayawingiani kuku.
  3. Mtama usioula wauwingiani ndege.
  4. Mzigo u kichwani kwapa lakutokeani jasho.
Post Views: 191
Kusikiliza na kuongea

Post navigation

Previous Post: Ufundishaji wa ufahamu
Next Post: Nahau

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme