Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Tanakali za sauti

Posted on By Harun Mbijiwe 6 Comments on Tanakali za sauti

Tanakali ni nini?

Hii ni tamadhali ya usemi ambayo hutumiwa kurejelea sauti inayoigiza jinsi kitu fulani kinavyotendeka. Tazama mifano ifuatayo:-

Tanbihi:

  • Usitenganishe sauti ya tanakali kwa mfano: lia kwi kwi kwi – inafaa lia kwikwikwi
  • Aidha usiweke alama ya mshangao mwishoni pa mlio. Kwa mfano: Lia kwikwikwi! Haya ni makosa inafaa lia kwikwikwi.

A

  1. Anguka kwa kitu chepesi kama vile penseli kacha.
  2. Anguka kwa mtu mnene bwata.
  3. Anguka kwa shilingi (chuma) sakafuni tangi
  4. Anguka majini chubwi.
  5. Anguka matopeni pwa.
  6. Anguka mchangani tifu.
  7. Anguka pahali pagumu pu.

B

  1. Bingirika bingiribingiri.
  2. Bwakia bwakubwaku
  3. Bweka bwebwebwe.

C

  1. Chapua miguu chapuchapu.
  2. Cheka kwakwakwa.
  3. Choka tiki.
  4. Churuzika churururu.

D

  1. Dondoka ndondondo.
  2. Dunda dududu.

E

  1. -eupe pepepe.
  2. -eusi pi/titititi.

F

  1. Funga ndindindi.
  2. Funika gubigubi.
  3. Furaha riboribo/furifuri/mpwitompwito.

G

  1. Giza totoro.
  2. Gugumiza gugugu

H

  1. Huzuni mpwitompwito.

J

  1. Jaa pomoni.
  2. Jaa sisisi.

K

  1. Kataa katakata.
  2. Komea komekome
  3. Kumbatiana papatu papatu.
  4. Kutopata ng’o

L

  1. Lala fofofo.
  2. Lewa ndi/chopi/chakari.
  3. Lia kwikwikwi.
  4. Lowa rovurovu/lovulovu/chepechepe.

M

  1. Maliza fyu.
  2. Matatizo tipitipi.
  3. Mchuzi rojorojo.
  4. Mulika mwaa.
  5. Mwagika mwa.

N

  1. Nuka fee/mff mff.
  2. Nukia hhh
  3. Nukia nhh.
  4. Nyamaza jii.
  5. Nyoka twaa.

P

  1. Pamba kochokocho.
  2. Ponea chupuchupu.
  3. Pukutika kupukupu.

R

  1. Regea regerege.
  2. Rowa rovurovu

S

  1. Saga tikitiki.

T

  1. Tafuna tafutafu.
  2. Teketea teketeke.
  3. Teleza parrr.
  4. Tiririka tiriri.
  5. Tokwa na jasho jekejeke.
  6. Tulia tuli.

V

  1. Vuma vuum.
  2. Vunjika kenyekenye.(kuvunjika kabisa)
  3. Vurugika vuruguvurugu.

Z

  1. Zimia zii.
Post Views: 199
Kusikiliza na kuongea

Post navigation

Previous Post: Nahau
Next Post: Mama Yangu Mpendwa

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme