Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Tashdidi

Posted on By Harun Mbijiwe 6 Comments on Tashdidi

Tashdidi ni fani ya lugha inayotumia maneno mawili yaliyo na maana moja kuleta msisitizo katika uandishi. Hizi ni kati ya tashdidi ambazo zimekusanywa kwa ustadi sitazokusaidia kupamba Insha yako vilivyo. Tazama mifano ifuatayo:-

  1. Adabu na nidhamu
  2. Akili na maarifa
  3. Alifoka na kung’aka
  4. Bidii na juhudi
  5. Bora na mufti
  6. Duwaa na kubung’aa
  7. Eleza na kufafanua
  8. Fika na kuwasili
  9. Fikiri na kutafakari
  10. Gundua na kufahamu
  11. Hamu na hamumu
  12. Haribu na kuvuruga
  13. Hasira na ghadhabu
  14. Heshimu na stahi
  15. Hiriki na kuangamiza
  16. Hofu na wahaka
  17. Imba na kughani
  18. Jaa na kufurika
  19. Jidai na kujinata
  20. Julisha na kufahamisha
  21. Kaa na kubarizi
  22. Kamsa na mayowe
  23. Karipia na kukemea
  24. Kelele na mayowe
  25. Kerwa na kereketwa
  26. Keti na kukaa
  27. Kubaliana na kuafikiana
  28. Kuchanganua na kupambanua
  29. Kufa na kufariki
  30. Kujisafisha na kujinadhifisha
  31. Kula na kushiba
  32. Kumbuka na kudhukuru
  33. Kumbuka na kutambua
  34. Kunionya na kunikanya
  35. Kuomba na kusihi
  36. Kuona na kuangalia
  37. Kupamba na kuremba
  38. Kwa dharau na bezo
  39. Lala na kusinzia
  40. Latifu na mpole
  41. Machugachuga na wasiwasi
  42. Majonzi na simanzi
  43. Maringo na madaha
  44. Mrembo na mlimbwende
  45. Mtiifu na mwadilifu
  46. Ng’aa na meremeta
  47. Nia na azma
  48. Nyamaza na kunyamaa
  49. Onya na kukanya
  50. Penya na kupenyeza
  51. Pigwa na kuchabangwa
  52. Polepole na taratibu
  53. Pongeza na kuongera
  54. Pongeza na kushukuru
  55. Safi na nadhifu
  56. Sema na kunena
  57. Sema na kukuli
  58. Shangaa na kubung’aa
  59. Shangaa na kusangaa
  60. Shikwa na kukamatwa
  61. Sikia na kusikiliza
  62. Subiri na kungojea
  63. Taabu na dhiki
  64. Tabasamu na kucheka
  65. Tafakari na kuvuta taswira
  66. Tambua na kung’amua
  67. Tamka na kusema
  68. Tembea na kuzurura
  69. Tiririka na kumwagika
  70. Toka na kutoweka
  71. Tosheka na kukinai
  72. Tua na kutulia
  73. Tuliza na kuliwaza
  74. Tunza na kuhifadhi
  75. Uliza na kusaili
  76. Uzuri na urembo
  77. Vaa na kuvalia
  78. Vishindo na vituko
  79. Vuta na kuburura
  80. Wasiwasi na shaka
  81. Wasiwasi na wahaka
Post Views: 242
Kusikiliza na kuongea

Post navigation

Previous Post: Jinamizi
Next Post: Insha za KCPE zilizotahiniwa tangia mwaka wa 1985 hadi 2023

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme