Skip to content

Kiswahili Mujarabu

Atangaye na jua hujua

  • Nyumbani
  • Yaliyomo
    • Sarufi
    • Kuandika
      • Utahini wa Insha KCPE
      • Insha Mbalimbali
      • Aina za insha
    • Kusikiliza na kuongea
    • Msamiati
    • Kusoma
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Toggle search form

Vitendawili

Posted on By Harun Mbijiwe 6 Comments on Vitendawili

Haya ni maneno yanayoficha maana ya kitu ili kisijulikane kwa urahisi. Nimeweka vichache ili kuweza kujifundisha.

A

  • Adui lakini popote huendako yuko nawe – nzi
  • Adui tumemzunguka lakini hatumuwezi – moto
  • Afahamu kuchora lakini hajui achoracho – konokono
  • Afuma hana mshale – nungunungu
  • Ajenga ingawa hana mikono – mchwa 
  • Ajenga ingawa hana mikono – ndege
  • Ajifungua na kujifunika – mwavuli
  • Ajihami bila silaha – kinyonga
  • Akibeba watoto wake hawezi kuwashusha – mahindi.
  • Akijikunja anakuwa herufi O akijinyoosha anakua namba moja – jongoo
  • Akimchukua hamrudishi – kaburi (kifo).
  • Akitokea watu wote humwona – jua
  • Akitokea watu wote hunungunika na kuwa na huzuni – ugonjwa
  • Akivaa nguo hapendezi, akiwa uchi apendeza – mgomba
  • Alipita mtu ana bunda la mshale – mkindu
  • Alipita mtu mwenye kibandiko cha nguo – inzi
  • Aliwa, yuala; ala, aliwa – papa
  • Amchukuapo hamrudishi – kaburi
  • Amefika kabla mjumbe hajarudi – nazi 
  • Amefunika kote kwa blanketi lake jeusi – giza
  • Amefunua jicho jekundu – jua
  • Ameingia shimoni akiwa uchi, akatoka amevaa nguo nzuri – mbegu
  • Amejiingiza jela mwenyewe – kuku akiatamia.
  • Amejitwika mzigo mkubwa kuliko yeye mwenyewe – konokono / Koa
  • Amekaa kimya na watoto wamemzunguka pande zote – mgomba
  • Amekula ncha mbili – wali
  • Amevaa joho kubwa kuliko yeye mwenyewe – kaburi
  • Ana mdomo lakini anang’ata kwa mkia – nge 
  • Ana miguu ya msumeno – panzi 
  • Anajua kuchora ingawa hajui anacho kichora – konokono 
  • Anakuangalia tu wala halali au kutembea – picha
  • Anakula kila siku lakini hashibi na hatashiba – mchanga
  • Anakula lakini hajashiba na hatashiba milele – ardhi
  • Anakula lakini hashibi – mauti
  • Anapendwa sana ingawaje ni mkali sana – moto
  • Anatengeneza mchuzi mtamu lakini hapiki jikoni – kivuli 
  • Anatoka kutembea, anakuja nyumbani anamwambia mama, ‘Nieleke’ – kitanda
  • Ashona mikeka wala hailali – maboga
  • Askari wangu ni mpole lakini adui wanamhara – paka
  • Askari wangu wote wamevaa kofia upande – majani
  • Askari wangu wote wamevaa mavazi meusi – chunguchungu
  • Asubuhi atembea kwa miguu mine, adhuhuri kwa miwili – fedha
  • Atapanya mbegu nyingi sana lakini hazioti – mvua
  • Atolewapo nje hufa – samaki

B

Babu amelala ndani ndevu zake zipo nje – mahindi  

Babu amevaa koti la chuma – kobe  

Bibi hatui mzigo wake – kobe / konokono

Bomu la machozi baridi – moshi  

Bwana afya wa pori – fisi  

C

Cheupe kimevunjika imetokea manjano – yai   

F

Fuu funika, fuu funua – kutembea  

G

Gari langu halitumii mafuta – miguu  

H

Hana staha wala adabu kwa watu – utelezi

Hapotei hata akiwa gizani – tonge mdomoni

Hausimiki hausimami – mkufu  

Hesabu yake haina faida – nywele / mchanga

Huku na huku tamu, katikati chungu – jua  

Huku ng’o na huko ng’o – giza  

Huuawa kwa uzazi wake – kinyonga

J

Jinamizi laniita lakini silioni – mwangwi  

Juu mboga, katikati kuni, chini ugali – mhogo

K

Kaa hapa na mimi nikae pale tumfinye mchawi – kula ugali

Kafa huku akining’inia – buibui

Kamba yangu ndefu lakini haiwezi kufunga mzigo wa kuni – barabara / njia

Kila mtu atapita mlango huu – kifo  

Kila mtu humwabudu apitapo – mlango

Kila niendapo hunifuata – kivuli  

Kila ukiwakuta wamejitayarisha kupigana – katani / mkonge

Kilemba chake hazimishi – jogoo

Kiota chanke kimezungushiwa boma la nyasi – macho

Kipara cha babu kinafuka moshi – ugali

Kondoo wetu ana nyama nje na ngozi ndani – firigisi

Kuku wangu hutagia miibani – nanasi

Kulia kwake ni kicheko kwetu – mvua  

M

Mama hachoki kunibeba – kitanda

Maskini huyu hata amechangiwa vipi haridhiki – tumbo.

Mazishi yake ni furaha kwa watu – mbegu  

T

  • Taa ya bure – Jua au mwezi
  • Taa ya Mwarabu inapepea – Kilemba
  • Tajiri aniweka mfukoni na maskini anitupa. Makamasi
  • Tandika kitanga tule kunazi. Nyota
  • Tangu kuzaliwa kwake sijamwona asimame wala kukimbia – Mkufu
  • Tatarata mpaka ng’ambo ya mto – Utando wa baibui
  • Tatu tatu mpaka pwani – Mafiga
  • Tega nikutegue – Mwiba
  • Teke teke huzaa gumugumu, na gumugumu huzaa teke teke – Mahindi ama yai
  • Tajiri wa rangi – kinyonga  
  • Teketeke huzaa gumu gumu, gumu gumu huzaa teke teke – mahindi
  • Tengeneza kiwanja kikubwa kabila Fulani lije kupigania – Mbono
  • Tonge la ugali lanifikisha pwani – Jicho
  • Tukate kwa visu ambacho hakitakatika – Maji
  • Tulikaribishwa mahali na mdogo wangu, yeye akaanza kushiba kabla yangu – Kucha
  • Tuliua ng’ombe na babu, kila ajaye hukata – Kinoo
  • Tuliua ng’ombe wawili ngozi ni sawasawa – Mbingu na nchi
  • Tumvike mwanamke huyu nguo – Kuezeka nyumba
  • Tunajengajenga matiti juu – Mapapai
  • Tunakwenda wote tunarudi wote lakini hatuongei – kivuli.
  • Twamsikia lakini hatumwoni – Sauti

U

  • Ubwabwa wa mwana mtamu – usingizi  
  • Ukimcheka atakucheka, ukimwomba atakuomba – mwangwi
  • Ukimwita kwa nguvu hasikii, lakini ukimwita polepole husikia – fisi
  • Ukimwona anakuona – jua
  • Ukitaka kufahamu ana mbio, mwonyeshe moto – kinyonga
  • Ukitembea ulimwengu wote utakosa nyayo – mwamba
  • Ukiukata haukatiki, ukiushika haushikiki – moshi
  • Ukiwa mbali waweza kumwona Fulani umatini – tundu la sindano
  • Ukoo wa liwali hauna haya – wanyama
  • Ule usile mamoja – kifo
  • Umempiga sungura akatoa unga – funda la mbuyu
  • Unatembea naye wote umjiao atakuona – bakora
  • Upande wote umjiao atakuona – kinyonga
  • Ushuru wa njia – Kujikwaa
  • Utahesabu mchana na usiku na hutamaliza kuhesabu – nywele
  • Ukisogea naye husogea, ukisimama naye husimama – kivuli  
  • Ukoo wetu hauishiwi na safari – siafu
  • Ukumbuu wa babu ni mrefu – barabara / njia
  • Utupacho wewe kwake ni dhahabu – nzi
  • Viti vyote nimevikalia isipokuwa hicho – moto

W

  • Wake wa mjomba kimo kimoja – vipande vya kweme
  • Wakikua mama yao huwatupa mbali kwa kishindo – mbarika / nyonyo
  • Wako karibu lakini hawasalimiani – nyumba ama kuta zinazoelekeana
  • Waliobeba maiti hawaongei lakini yeye anaongea – chungu kinapochemka
  • Wana wa mfalme ni wepesi sana kujificha – macho
  • Wanakuja mmoja mmoja na kujiunga kuwa kitu kimoja – matone ya mvua
  • Wanameza watu jua linapokuchwa – nyumba
  • Wanamwua nyoka – watu wanaotwanga
  • Wanangu wawili hugombana mchana, usiku hupatana – mlango
  • Wanao wakati wao wa kuringa, nao ni weupe kama barafu – nyota
  • Wanapanda mlima kwa makoti mazuri meusi na meupe – vipepeo
  • Wanastarehe darini – panya
  • Wanatembea lakini hawatembelewi – macho
  • Watoto wa binadamu wakiondoka hawarudi – majani    
  • Watoto wa mtu mmoja hulala chini kila mwaka – maboga
  • Watoto wa tajiri wa nguo hulala na kutembea uchi – maboga
  • Watoto wangu wana vilemba, asio kilemba si mwanangu – fuu
  • Watoto wangu wote nimewavika kofia nyekundu – jogoo
  • Watoto wangu wote wamebeba vifurushi – vitovu
  • Watu waliokaa na kuvaa kofia nyekundu – kuku, katani au mahindi
  • Watu wamehama askari wekundu wakazidi nyikani – viroboto
  • Watu wote ketini tumfinye mchawi – kula ugali
  • Wewe kipofu unaenda wapi huko juu? – kweme   

Y

  • Yaenda mbali lakini haiondoki ilipo – njia

Z

  • Zilitazamana na mpaka sasa hazijakutana – kingo  za mto
  • Ziwa dogo linarusha mchanga – chungu  jikoni
  • Ziwa kubwa, lakini naogelea ukingoni tu – moto
  • Zulia la Mungu – ardhi.
Post Views: 455
Kusikiliza na kuongea

Post navigation

Previous Post: Abjadi, abtathi au alfabeti
Next Post: Aina za Vitenzi

Machapisho mapya

  • Barua
  • Insha ya Methali
  • Tashbihi
  • Ngeli na maelezo yake
  • Hotuba

Kumbukumbu

  • June 2025
  • January 2025
  • May 2024
  • February 2024
  • January 2024
  • September 2023
  • July 2023
  • April 2023
  • March 2023
  • September 2021
  • August 2021
  • July 2021
  • June 2021

Kategoria

  • Aina za insha
  • Insha Mbalimbali
  • Kusikiliza na kuongea
  • Kusoma
  • Majibu
  • Mawaidha ya Ufundishaji
  • Msamiati
  • Sarufi
  • Utahini wa Insha KCPE

Copyright © 2025 Kiswahili Mujarabu.

Powered by PressBook Green WordPress theme